ADDY...MOTO WA BONGO FLAVOUR TOKA NJOMBE
Na: Kalmas Konzo
Najua utasema humfahamu...Basi ngoja nikufahamishe...Jamaa anaitwa ADDY
aka BROTHER... Ni mwanamuziki mkali wa miondoko ya BONGO FLAVOUR toka
mkoani NJOMBE... Mwanamuziki huyu amebarikiwa kipaji cha pekee ikiwa ni
sambamba na sauti tamu ya pekee ambayo haichoshi kuisikiliza.
Ni miaka kadhaa sasa imepita toka nimfahamu ADDY. Kwa mara ya kwanza nilipokutana naye nilitambua fika kwamba kijana huyu atafika mbali sana katika tasnia hii ya kizazi kipya hapa nyumbani Tanzania.
Ana kila sababu ya kupewa pongezi za dhati kutokana na kazi nzuri anazozifanya. Ukibahatika kuzisikiliza kazi zake utanielewa ni nini ninachokizumgumzia.
Kwa sasa anakuja na albamu akiwa anatesa na video yake ya UA... Karibuni sana mumpokee
No comments:
Post a Comment