For home theatre system solution

Friday, February 17, 2012

DAR ES SALAAM

Bifu la Isha Mashauzi, Rahma ni noma

Posted by GLOBAL on February 17, 2012 at 9:30am 3 Comments


Na Rhobi Chacha

Bifu kati ya Mkurugenzi wa kundi la muziki wa mwambao la Mashauzi Classic Morden Taarab, Aisha Ramadhani ‘Isha Mashauzi’ (pichani) na muimbaji wa Jahazi Modern Taarab, Rahma Machupa ni noma kutokana na madai eti Rahma anadaiwa na Isha kuwa ‘anabinjuka’ na Thabit Abdul ‘Baby.’

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho ndani ya kundi hilo, tuhuma za wawili hao kupeana ‘mambo’ zipo kitambo.

Kufuatia madai hayo, mwandishi wetu alimtafuta Rahma na kufanya naye mahojiano ambapo alifunguka:

“Kwanza napenda ieleweke kuwa nimejitoa Mashauzi Classic na…


Na Rhobi Chacha
Bifu kati ya Mkurugenzi wa kundi la muziki wa mwambao la Mashauzi Classic Morden Taarab, Aisha Ramadhani ‘Isha Mashauzi’ (pichani) na muimbaji wa Jahazi Modern Taarab, Rahma Machupa ni noma kutokana na madai eti Rahma anadaiwa na Isha kuwa ‘anabinjuka’ na Thabit Abdul ‘Baby.’
Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho ndani ya kundi hilo, tuhuma za wawili hao kupeana ‘mambo’ zipo kitambo.
Kufuatia madai hayo, mwandishi wetu alimtafuta Rahma na kufanya naye mahojiano ambapo alifunguka:
“Kwanza napenda ieleweke kuwa nimejitoa Mashauzi Classic na kuhamia Jahazi Modern Taarab, sababu kubwa ni maneno ya Isha kunishutumu kuwa natoka kimapenzi na Thabiti,” alisema msanii huyo.
Mashauzi aliposomewa mashtaka yake kuhusu madai hayo alisema hayana ukweli wowote.
“Unajua ukubwa ni jalala, hakuna kitu kama hicho, huyo Rahma anasema uongo tu labda anajua akiongea hivyo atapata umaarufu mapema kumbe anajiharibia,” alisema Isha.
Thabiti anayetuhumiwa kuchangia kuwepo kwa bifu kati wadada hao alipotafutwa alisema, yeye anatuhumiwa tu ila ukweli ni kwamba hana uhusiano na Rahma wala Isha kama inavyodaiwa.

No comments:

Post a Comment