Na Sandahillary Mnyawusuha
- TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,
amewateua wafuatao kuwa Wakuu wa Mikoa .
Dkt. Rajab Mtumwa Rutengwe ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa KATAVI . Kabla ya hapo Dkt. Rutengwe alikuwa Mkuu wa wilaya ya Mpanda.
Ndugu Magalula Saidi Magagula ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa GEITA . Kabla ya hapo Ndugu MAGALULA alikuwa Mkuu wa wilaya ya Lindi.
Ndugu Paschal Kulwa Mabiti ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa SIMIYU . Kabla ya hapo Ndugu MABITI alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Singida.
Kapt. Asery Msangi ameteuliwa kuwa Mkuu wa
Mkoa wa NJOMBE . Kabla ya hapo Kapt. MSANGI alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa.
Uteuzi huu unaanza tarehe 15 Machi, 2012 . Wataapishwa Ikulu, Dar es Salaam, Jumatano tarehe 21 Machi, 2012 saa 04:00 asubuhi .
Imetolewa na : Kurugenzi ya Mawasiliano ya
Rais, Ikulu . Dar es Salaam. 15 Machi, 2012