For home theatre system solution

Tuesday, February 21, 2012

BREAKING NEWS

SUGU NA RUGE MUTAHABA WAPATANA



Hatimaye ugomvi wa Ruge Mutahaba na Mbunge wa jimbo la Mbeya kwa tiketi ya CHADEMA Mh. Joseph Mbilinyi (Sugu) umekwisha baada ya kufanyika kwa vikao mbali mbali chini ya Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, John Nchimbi na Mbunge Tundu Lisu.

Chanzo: www.djfetty.blogspot.com

NIGERIA

Jeshi la Polisi Nigeria lawauwa Boko Haram
 
 
Walinda usalama katika mji wa Maiduguri

Msemaji wa jeshi la Nigeria amesema kwamba wanajeshi watatu walijeruhiwa katika
makabiliano hayo ya risasi na kundi la Boko Haram.

Hata hivyo alikanusha kuwa kuna raia yeyote aliyeuwawa katika kisa hicho.

Lakini wenye maduka katika soko la Baga wamenukuliwa wakisema kuwa wameona maiti zipatazo ishirini hivi zikipakiwa kwenye lori.

Eneo hilo la Maiduguri ni ngombe kuu ya wapiganiaji wa Boko Haram . Na katika miaka ya hivi karibuni sehemu imeshuhudia milipuko kadhaa na ufyatuliananji wa risasi.

Tayari serikali ya rais Goodluck Jonathan imetangaza hali ya hatari katika mji huyo na miji menginea ambayo imeshuhudia mashambulizi toka kwa kundi hilo la Boko Haram.

Lakini wakazi wa miji hiyo wanasema kuwa suluhu ya kijeshi haijafaulu leta mafanikio yeyote

Chanzo: Global Publishers

NJOMBE

ANNA MAKINDA AWAASA WANANCHI WA NJOMBE

Na Kalmas Konzo
Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mbunge wa jimbo la Njombe kusini Mheshimiwa Anna Makinda amewataka wakazi wa Njombe kuwa wafanye kazi kwa bidii kuweza kuyafikia mafanikio katika maisha yao.

Mheshimiwa Anna Makinda ameyasema hayo pindi alipokuwa akizungumza na wananchi wa Idundilanga katika kata ya Njombe mjini.

Anna Makinda amewataka wananchi waache kupiga soga vijiweni pasipo kufanya kazi kwani mafanikio hayawezi kuletwa na uvivu wa kutokufanya kazi.

Amewataka wananchi kuzitumia fursa zinazopatikana kama mradi wa Mchuchuma na Liganga katika kufanya kazi kwa bidii kwani fursa hizi huwa hzijitokezi mara mbili. Amewaasa kuwa fursa kama hizo zitaweza kuwaletea mafanikio wao wenyewe na mkoa wa Njombe kwa ujumla.

Copy right: www.tuburudike.blogspot.com