ANNA MAKINDA AWAASA WANANCHI WA NJOMBE
Na Kalmas Konzo
Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mbunge wa jimbo la Njombe kusini Mheshimiwa Anna Makinda amewataka wakazi wa Njombe kuwa wafanye kazi kwa bidii kuweza kuyafikia mafanikio katika maisha yao.
Mheshimiwa Anna Makinda ameyasema hayo pindi alipokuwa akizungumza na wananchi wa Idundilanga katika kata ya Njombe mjini.
Anna Makinda amewataka wananchi waache kupiga soga vijiweni pasipo kufanya kazi kwani mafanikio hayawezi kuletwa na uvivu wa kutokufanya kazi.
Amewataka wananchi kuzitumia fursa zinazopatikana kama mradi wa Mchuchuma na Liganga katika kufanya kazi kwa bidii kwani fursa hizi huwa hzijitokezi mara mbili. Amewaasa kuwa fursa kama hizo zitaweza kuwaletea mafanikio wao wenyewe na mkoa wa Njombe kwa ujumla.
Copy right: www.tuburudike.blogspot.com
No comments:
Post a Comment