For home theatre system solution

Monday, February 20, 2012

MAREKANI

DMX AVAMIWA APIGWA NONDO KICHWANI

Kijana mtanashati mjini Iringa maarufu kwa jina la DMX amenusurika kifo baada ya kuvamiwa na vijana ambao amewatambua kwa majina na kumjeruhi kwa kumpiga nondo kichwani ,DMX alivamiwa usiku wa juzi eneo la Makorongoni katika Manispaa ya Iringa
 
Chanzo: www.francisgodwin.blogspot.com

DAR ES SALAAM

KUONA MECHI YA STARS NA DRC TSH 2,000


Kiingilio kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya Taifa Stars na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) itakayofanyika Februari 23 mwaka huu kitakuwa sh. 2,000 kwa viti vya kijani na bluu.
 
Mechi itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo viti hivyo vya kijani na bluu vinachukua watazamaji 36,693 ambayo ni karibu theluthi mbili ya viti vyote kwenye uwanja huo wa kisasa.
 
Viti vya rangi ya chungwa kiingilio ni sh. 5,000, VIP C itakuwa sh. 7,000 wakati VIP B tiketi zitauzwa kwa sh. 10,000. Kiingilio kwa viti vya VIP A kitakuwa sh. 15,000.
Kwa vile Februari 23 mwaka huu ni siku ya kazi ili kutoa fursa kwa washabiki wengi kushuhudia pambano hilo la kimataifa, mechi hiyo itaanza saa 11 kamili jioni.
 
Wakati Taifa Stars inayofundishwa na Jan Poulsen imeingia kambini leo na ikitarajiwa kuanza mazoezi jioni kwenye Uwanja wa Karume, DRC ambayo iko chini ya kocha Claude Le Roy inatarajia kutua nchini kesho.
 
Taifa Stars na DRC zinatumia mechi hiyo kunoa wachezaji wao kabla ya mechi zao za mchujo za Kombe la mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini. 
 
Katika raundi hiyo ya awali ambayo mechi zake zitachezwa Februari 29 mwaka huu, Stars itaanzia nyumbani dhidi ya Msumbiji wakati DRC inaanzia ugenini dhidi ya Seychelles.
 
Chanzo: francisgodwin.blogspot.com
 

IRINGA

INATISHA NI BAADA YA KUSHINDWA KUUA AJICHOMA KISU SHINGONI

Mwanamke ambae bado hajafahamika jina wala anakoishi katika mkoa wa Iringa akiwa hoi baada ya kujichoma kisu shingoni mwenyewe kwa kile kinachodaiwa kuwa ni baada ya mwenyeji wake kumkimbia na kujificha chooni kukwepa kuuwawa na mwanamke huyo asubuhi ya leo eneo la Frelimo mjini Iringa(picha zinatisha sana naomba radhi kwa usumbufu )
Hapa akikimbizwa hospitali ya mkoa na askari polisi waliofika kunusuru maisha yake

Chanzo: francisgodwin.blogspot.com