For home theatre system solution

Thursday, March 22, 2012

LUDEWA

  •  HATIMAYE DIWANI ALIYEJINYONGA LUDEWA AZIKWA
    Na Godlove Mtokambali
    Mheshimiwa diwani Rudolf Chaula ambaye alijinyonga ofisini kwake amezikwa jana tarehe 22/03/2012 katika makaburi ya kanisa katoliki kata ya mlangali. 
     
    Umati mkubwa sana ulifurika kumsindikiza marehemu katika makazi yake ya mwisho, ukiwemo uongozi wa wilaya ya Ludewa na madiwani wa kata mbali za Ludewa. 
     
    Inasadikika kwamba marehemu alijinyonga baada ya kudhukumiwa kiasi cha shilingi milioni 81.
     
    Mwendesha msiba alisoma kikaratasi alichokiacha marehemu ambacho kinadai kati ya shilingi milioni 81 alizodhulumiwa, milioni 41 zilikuwa ni mali ya SACCOS Mlangali na milioni 40 ni mali ya familia ya marehemu. 
     
    Uongozi wa kanisa katoliki uligoma katakata kuuombea mwili wa marehemu. 
     
    Marehemu alijinyonga usiku wa kuamkia majuzi katika mojawapo ya vyumba anavyotumia kama ofisi yake ya udiwani kwa kamba ya mbuzi.

No comments:

Post a Comment